Mchungaji wa kanisa mbaroni kwa mauaji Mwanza

MCHUNGAJI wa kanisa la Tanzania Adventist Conference (TACC) lililopo kata ya Kiseke, Ilemela mkoani Mwanza, Hanscolling Exaud (Munuo) anatuhumiwa ya Samwel Makoye.

Tukio hilo lilitokea jana saa 11 alfajiri wakati marehemu huyo ambaye alikuwa mchungaji wa ng’ombe alipoingia katika shamba la mtuhumiwa na kuanza kushambuliwa na mchungaji huyo wa kanisa kwa mpini wa jembe mwilini.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza, Kamishna Mwandamizi Msaidizi, Charles Mkumbo, amesema Makoye akiwa anakata majani aina ya matete kwa ajili ya kulishia ng’ombe, ghafla alivamiwa na Munuo na kuanza kushambuliwa hadi alipopoteza fahamu na mtuhumiwa huyo kukimbia.
Mkumbo amesema marehemu Makoye alifanikiwa kupiga kelele ambazo zilisaidia majirani kufika eneo la tukio, lakini kwa kuwa alikuwa hajiwezi kutokana na kipigo na alipoulizwa aliyemfanyia ukatili huo, alimtaja mchungaji Munuo.
“Baada ya wananchi kuelezwa hayo na marehemu ndipo walilitaarifu jeshi la polisi na kumpeleka hospitali ya Rufaa ya Bugando (BMC) kwa matibabu lakini alifariki saa moja baadaye,” amesema Mkumbo.
Kufuatia taarifa hizo, polisi walifanikiwa kumtia mbaroni mchungaji huyo na kukiri kumpiga mkata majani huyo ambaye ni mwajiri wa Holiday David, kutokana na kuvamia eneo la shamba lake kwa kukata majani ya ng’ombe.
Kamanda Mkumbo aliwataka wananchi kutojichukulia sheria mkononi kama alivyofanya mchungaji huyo ambaye atafikishwa mahakamani baada ya uchunguji kukamilika.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo