MTIA NIA UBUNGE LUDEWA AWATIBUA WANANCHI WAMZOMEA BAADA YA KUAHIDI KUJENGA BENKI YA WILAYA KILA KIJIJI

Deo Filikunjombe na watia nia wengine wa ubunge jimbo la Ludewa wakiwapungia mikono wananchi wa Luilo leo walipofika kujinadi kwao .......................................................................... 
Na Matukiodaima BLOG 

BAADA ya jana kuzomewa na kunusurika kichapo kabla ya kushushwa jukwaani kwa nguvu kutokana na kubeza kazi kubwa za kimaendeleo zilizofanywa na mbunge Deo Filikunjombe katika jimbo hilo la Ludewa mtia nia ubunge kupitia chama cha mapinduzi kepteni mstaafu Jacob Mpangala azidi kulikoroga kwa wananchi baada ya wananchi wa kata ya Iwela na Luilo kumpinga hadharani kutokana na ahadi yake yakujenga benki ya wananchi Ludewa kila kijiji cha jimbo hilo. 

Pamoja na kupinga vikali ahadi hiyo walioiita ni ahadi ya kuwadanganya pia wananchi hao walimpinga mtia nia huyo kuwa ni muongo kufuatia kauli yake ya kudai kuanzisha kilimo cha umwagiliaji katika kata ya Luilo na Iwela wakati katika maeneo hayo ni milima. 

Mtia nia huyo ambae anatokea eneo la Manda kando ya ziwa nyasa baada ya kubanwa juu ya nini amekifanya katika wilaya hiyo ya Ludewa alijikuta akizomewa kwa mara ya pili na hata wananchi kususa kuendelea kumsikiliza baada ya kudai kuwa yeye ndie aliyeanzisha kambi ya jeshi Mada wakati katika maelezo yake akidai kuwa alistaafu kazi ya jeshi mwaka 2008 na kambi hiyo imeanzishwa mwaka huu. 

Wananchi hao ambao ni wanachama wa CCM walidai kuwa wamelazimika kuondoka katika mkutano huo baada ya kumsikiliza mbunge wao Filikunjombe na kuridhishwa na ahadi zake na kazi alizozifanya ila wamemuona mtia nia huyo anawadanganya kwa kuwapotezea muda bure kwani wanachoamini wao kazi ya kuwaondoa hofu wananchi wa mwambao mwa ziwa nyasa juu ya kauli za aliyekuwa rais wa Malawi wakati huo Joyce Banda aliyekuwa akitishia kutaka kumiliki ziwa hilo lote ilifanywa na mbunge wao ambae alikuwepo madarakani na mtia nia huyo kwa wakati wa mgogoro huo mwaka jana hakuwepo kazini . 

‘’ Ni kweli ndani ya CCM kuna demokrasia ya kila mwenye sifa kujitokeza kugombea ila tunachokiona kwa hawa wagombea wawili waliojitokeza kumpinga mbunge wetu Filikunjombe ni wazi wametumwa na mafisadi kuja kutaka kutuvuruga na mbaya zaidi hawana jipya la nini watafanya na ndio sababu wanatumia muda mwingi kutudanganya kwa kuokoteza sera za uongo ……..tunasema hatudanganyiki na hawa wanaokuja wakati wa uchaguzi wananchi wa Ludewa hawana shida ya kuchagua mbunge mpya nje ya jembe lao Filikunjombe kwani huyo injinia zephania chaula hii ni mara ya tatu anagombea ila akikosa huwa haonekani tena hadi mwaka wa uchaguzi tunasema mwaka huu hatudanganyiki na ili kuwaonyesha kuwa wana Ludewa tupo na jembe letu mwaka huu tutawachapa kweli’alisema John Haule . 

Huku Jane Lukuwi akidai kuwa wana ya uongozi wake wameyaona na kuongeza kuwa watia nia hao wawili wote katika maelezo yao wanakubali kutumwa kugombea ubunge na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo prof Raphael Mwalyosi ambae walimuacha baada ya kushindwa kufanya kazi za kimaendeleo kwa kipindi chote cha miaka mitano hivyo kama wao walivyojichagulia mbunge bora mwaka 2010 hawana shida ya kuchaguliwa mbunge na mbunge aliyeachwa kwa kutowatumikia wananchi. 

‘’Hawa wagombea wawili tunawashangaa sana wanaposema wametumwa na mbunge prof Mwalyosi na kutamka hadharani kuwa mbunge wao Filikunjombe atakatwa na vikao vya juu vya CCM tena bila kujizuia wanadai kuwa juu kuna mjumbe mzito wa vikao vya maamuzi ambae yupo nyuma yao ….tunaomba kukiomba chama tawala wakitaka kujua wao wanauamuzi gani juu ya jembe lao Filikunjombe basi waruhusu huyo kigogo wa juu wa vikao vya maamuzi kupokonya haki yao kwa kukata jina la jembe letu ‘’leo kijiji cha Luilo 

Kwa upande wake mbunge Filikunjombe akijinadi kwa wananchi hao mbali ya kuwashukuru kwa kuendelea kuonyesha imani kubwa kwake bado alisisitiza kuwa kamwe hatasinzia bungeni kama walivyofanya baadhi ya wabunge wenzake na kuwa siku zote ataendelea kupigania maendeleo ya jimbo la Ludewa na kuwa kwa vile bado anaupenda ubunge na anawapenda wana Ludewa hataacha kuendelea kushirikiana nao kuleta maendeleo. 

Alisema hadi sasa anajivunia maendeleo makubwa ambayo ameyafanya katika jimbo hilo yakiwemo ya umeme vijjini , uboreshaji wa miundo mbinu ya barabara , huduma za afya, kupigania masoko bora ya mazao kwa wakulima, kusomesha yatima 25 kila kata ya jimbo hilo kwa kila mwaka na maendeleo mengine mengi ambayo sasa yanawavutia wana Ludewa kutembea kifua mbele tofauti na awali ambapo baadhi yao walikuwa wakikwepa wilayani hiyo . 

‘’Ninatambua wazi kuwa wananchi wangu mnanipenda na mimi nawapenda zaidi hivyo ili tuzidi kusonga mbele zaidi na kuonyesha kuwa mnanipenda nawaombeni mnipeni kura zote hata kwani baada ya kazi nzuri ya maendeleo hawa wenzangu wawili wamejitokeza kunisindikiza na ndio maana kila wanapokwenda wanaishia kupingwa kutokana na haya maelezo yao kuwa wametumwa kunitoa madarakani '' 

Mvuto wa watiania hao wawili umezidi kupungua zaidi kutokana na wananchi ahadi zao ambazo zinapelekea wananchi kuwapinga kila mkutano hasa ahadi ambayo wananchi wamekuwa wakipinga na hata kuwazomea ile ya kujenga benki ya wananchi wa Ludewa kila kijiji kwa vijiji vyote zaidi ya 76 pamoja na kuanzisha miji midogo kila kijiji pia kuanzisha kilimo cha umwagiliaji katika vijiji huku wananchi wakitambua wazi kuwa Jogrofia ya Ludewa ni milima zaidi hivyo kutokana na sera za watiania hao kuwakwaza wamekuwa wakijikuta wakivunja kanuni za mikutano hiyo ya kutokushangilia wala kuzomea na kujikuta wakizomewa kila mkutano


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo