MILIONI 50 KUTOLEWA KWA ATAKAYEFANIKISHA KUKAMATWA MAJAMBAZI WALIOVAMIA STAKISHARI

JESHI la Polisi nchini leo limetangaza zawadi nono ya shilingi milioni 50 kwa mtu yeyote atakayefanikisha kukamatwa kwa majambazi waliovamia Kituo cha Polisi cha Stakishari kilichopo Ukonga, Dar juzi.

Zawadi hiyo imetangazwa leo jijini Dar na Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleimani Kova kwa niaba ya jeshi hilo.

Majambazi hao walivamia Kituo cha Polisi cha Stakishari kilichopo Ukonga, Dar juzi usiku na kuua watu saba wakiwemo askari wanne, raia wawili pamoja na jambazi mmoja aliyeuawa na wenzake hao kisha kupora silaha.
(Habari: Gabriel Ng'osha / GPL)


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo