LEO NI LEO HUKO DODOMA, CCM KUANZA KUNYOA AU KUSUKA

Mwenyekiti wa chama hicho Rais Jakaya Kikwete atastaafu baada ya uchaguzi huo akiwa amemaliza muhula wake wa pili na wa mwisho madarakani, kwa mujibu wa Katiba.
Maafisa wa ngazi ya juu wa chama hicho watawachagua wagombe watatu, ambao hatimae watapigiwa kura katika mkutano mkuu Julai12 kumpata mgombea Urais.
Miongoni mwa wanasiasa wanaotajwa zaidi ni Makamu wa Rais Mohamed Gharib Bilal, Waziri mkuu Mizengo Pinda, Jaji mstaafu Agustino Ramadhani, Waziri wa mambo ya nchi za nje Benard Membe na Waziri mkuu Mstaafu Edward Lowassa.
Pia katika orodha ya wagombea 39 yumo waziri wa sheria aliyewahi kuwa naibu katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Asha Rose Migiro.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo