Lediana Mng'ong'o aukosa Ubunge, aangukia pua kura za maoni Iringa

Macho yaliyojaa mbubujiko wa Machozi na Nyuso za Huzuni miongoni mwa wagombea Ni mara baada ya kutangazwa majina mawili yaliyopita kidedea miongoni mwa majina tisa ya wagombea Ubunge wa Viti maalum wanawake mkoani Iringa ambao walitumia haki yao ya msingi Katika kugombea nafasi hiyo ambapo baada ya kura kupigwa na wajumbe wa mkutano Mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania mkoani Iringa na Kuwafanya Rose Tweve na Aliyekuwa Mbunge wa Viti maalum mkoani kutetea kiti chake kwa kupitishwa kwa mara nyingi kuwaongoza wanawake hao. 

Uchaguzi wa Wabunge wa Viti maalumu ulifanyika ijumaa ya tarehe 24/07/2015 katika ukumbi wa St Dominic Iringa Mjini ambapo jumla ya wajumbe Katika mkutano huo ni zaidi ya 375 ambao ni wapiga kura halali. 

Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo msimamizi mkuu wa uchaguzi huo ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mh Amina Masenza alisema kura zilizopigwa zilikuwa 375,zilizoharibika ni 5,ambapo aliwataja wagombea na kura walizopata,alimtaja Agnesy Nyakunga (4),Farida Ninje(4),Hafsa Mtasiwa(10),Emma Mwalusamba(14),Esta Chaula(21), Shakira Kiwanga(89), Lediana Mng’ong’o(162), Ritta Kabati(199), Rose Tweve(240). 

Hivyo aliwatangaza washindi kwa mujibu wa katiba ua UWT kuwa wawakirishi wa wanawake Katika kipindi cha miaka mitano ijayo kuwa ni Rose Cyplian Tweve na Mh Ritta Kabati hivyo Katika mchakato huo wa kuwapata wawakilishi hao Mh Lediana Mng’ong’o ameshindwa kutetea nafasi yake baada ya kutopata kura za kutosha. 

“ndugu wajumbe niwashukuru sana kwa ushirikiano wenu naomba niwatangaze wawakirishi wenu kuwa ni Ndugu Rose Tweve na Ritta Kabati hivyo sasa wanahitaji sana wingi wa kura za Urais na Ubunge ndipo wataingia bungeni kwahiyo mnayokazi ya kufanya kuhakikisha tunakipa ushindi Chama Cha Mapinduzi huko tuendako Katika uchaguzi ujao”alisema msimamizi 

Wakizungumzia mchakato wa uchaguzi huo wagombea walisema wameridhishwa na mchakato huo pamoja wameridhia ushindi walioupata wagombea wengine na kuahidi kushirikiana nao kwa kila hali ili kuhakikisha Chama kinapata ushindi wa Kishindo. 

Akifunga mkutano huo mwenyekiti wa UWT mama Mwamwindi aliwapongeza wanawake wote kwa kuonyesha ukomavu wa siasa mara baada ya kwapata viongozi waliokuwa wakihitajika pia kuwasisitiza kuujenga roho ya Umoja miongoni mwao ili kukipa ushindi Chama.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo