PROF LIPUMBA ATANGAZA NIA YA KUGOMBEA URAIS KWA TIKETI YA UKAWA MWAKA HUU

Mwenyekiti wa umoja wa vyama vinavyounda UKAWA nchini na mwenyekiti wa chama cha wananchi (CUF) Mhe. Prof Ibrahimu Haruna Lipumba ametangaza nia ya kupeperusha bendera ya ukawa kwa  kugombea urais, katika uchaguzi mkuu ujao oktoba mwaka huu ili kupewa ridhaa na wananchi ya kuiongoza nchi ya Tanzania.

Akiwahutubia umati mkubwa wa wananchi katika viwanja vya Mwananchi Squer katika mji mdogo wa Urambo mwenyekiti wa UKAWA Ibrahimu Lipumba amesema kuwa, kama UKAWA utaamua kumpitisha mgombea mwingine atakuwa tayari kumpigia debe mteule wa UKAWA, lakini malengo yake ya kutaka kugombea urais, ni kutafuta haki ya wananchi ambayo imepotea.
 
Aidha katika hatua nyingine Mhe Prof Ibrahimu Lipumba amewataka watanzania kutambua kwa changamoto ambazo zinawakabili zikiwa ni upatikanaji wa haki za kijamii, zitaondolewa na rais ambaye atatoka nje ya chama cha mapinduzi na si vinginevyo, na kama hawatachagua rais kutoka nje ya CCM wajue hali ngumu ya maisha itaendelea kuwakabili kutokana na kutokuwepo na haki.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo