SAUTI YA FREEMAN MBOWE AKIMTAJA ALIYEMALIZA MGOMO WA MABASI UBUNGO

Mgomo wa Madereva ulimalizwa mchana wa May 5 2015 kwenye stand kuu ya Ubungo muda mfupi baada ya Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Paul Makonda pamoja na Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe kuwasili.
Baada ya hapo kwanza kulikua na taarifa kwenye mitandao mbalimbali kwamba Paul Makonda hakuhusika kumaliza mgogoro huo bali Mwenyekiti Freeman Mbowe.
Swala la mgomo wa madereva limekua na athari nyingi na tofauti kwa taifa na tangu mgomo umeanza jana watu mbalimbali wameathirika na upande wa pili bado ni ukweli tu kwamba hata madereva madai yao yana msingi na yanastahili kutatuliwa, kamati kuu ilinishauri nikaweze kuona naweza kuwa wa msaada gani’
Aliyefanya mazungumzo hasa rasmi na Madereva alikua ni mkuu wa wilaya ya Kinondoni Paul Makonda na nilipofika nilimkuta akiwa kwenye mazungumzo na viongozi wa madereva na kimsingi walikua walishaafikiana, nilichojaribu kukizungumza ni kuunga tu mkono kwasababu sikuona jambo baya lililofanyika na kuwatia moyo kwa upande huo’


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo