Na Andrew Chale wa Modewji blog
Huenda ulipata kusikia habari za Staa wa filamu za kibongo, ‘Bongo Movie’ Aunt Ezekiel ambaye kwenye mtandao wake wa kijamii wa Intagram anatumia IG Auntyezekiel, mapema asubui ya leo Aprili 30, kupitia IG hiyo ametupia picha ya tumbo lake. (Tazama picha hapo juu).
Hata hivyo katika picha hiyo, Aunty Ezekiel aliandika: ‘Morning…’ ikiwa ni sabahi kwa fans wake, ambaye hadi sasa ana fans walio m-follow 311K. huku akiwa na wastani wa kila post yake anayotupia IG, kupata LIKES nyingi zinazofikia zaidi ya 8,000 hadi 1,000.
Hata hivyo, hadi Mtandao huu unarusha Exclusive hii tayari post hiyo aliyoanika tumbo lake imeweza kufikisha LIKES zaidi ya 3,522 huku akipata Comments zaidi ya 394.( Likes na Comments zinaongezeka hii ni kwa muda tuliochukua taarifa).
Kama ilivyo kawada ya Mastaa wengi na watu maarufu kwa tabia ya kutojibu ama kurejea kubadilishana mawazo na fans wao, ambao kwa post hiyo wengi wa watu waliotembelea na kuchangia maoni yao wapo waliompongeza na kumuombea huku wengine wakimponda na kumtukana kwa kuwaonyeshea kitumbo hicho.
Modewji blog iliweza kubaini kuwa kutokana na Aunty Ezekiel kuwa na ukaribu na Wema Sepetu hali hiyo imefanya #teamDiamond kutembelea post hiyo na kurusha maneno ya vijembe huku wengine wakimtukana na kumpa ‘makavu Live’.
Baadhi ya waliochaangia akiwemo Magemmasi alimtupia dongo na kumuambia asimuige Hamisa Mabeto ambaye ni modol na aliwahi kupost picha kama hizo kupitia mitandao ya kijamii na baada ya siku mbili alijifungua na wengine wengi ambao maneno yao kwa maadili hatuwezi kupost hapa ila unaruhusiwa kum-follow kupitia IG yake ya auntyezekiel na kuona hayo yote.
Kimeeleweka:
Mtandao huu kupitia vyanzo mbalimbali vya habari viliweza kuwasiliana na wataalam wakiwemo madaktari ambao walieleza kuwa kwa kawaida mimba kitaalaamu huwezi ibashiria kitu hadi pale mama mjamzito anaposhikwa na uchungu na kisha kupelekwa leba hivyo hata kama tumbo lipo kubwa kiasi gani ama lipo dogo kiasi gani, kama ni mjamzito mwisho wa siku ni pale anapojisikia uchungu ndipo atakapokimbizwa leba na kujifungua.
Alijibu Daktaari huyo wa Kinondoni Hospita, hii ni baada ya kumuhoji juu ya athari anazoweza kuzipata mwanamke mjamzito pindi atakapokaa muda mrefu na ujauzito licha ya kuwa tumbo lake la mimba kuwa kubwa.
Mimba hiyo ya Aunt Ezekiel imekuwa ikifuatiliwa mara kwa mara na watu mbalimbali huku wakitaka kuona anajifungua ambapo miezi kadhaa iliyopita mitandao ya kijamii iliwahi kutoa taarifa za kujifungua kwa staa huyo ambaye pia anamvuto wa asili na asiyechuja tokea kuingia kwenye soko la filamu za kibongo.
Mose Iyobo katikati anayeelezwa kuwa ndiye ‘kidume aliyetundika mimba iyo’ kwa Aunty Ezekil (kulia), wa kusoto ni rafiki yao.
Hata hivyo, kikubwa cha watu wengi wakiwemo fans wake kumsubiria ajifungue, ni kuona mtoto huyo ni wa nani licha ya kuwa tayari Mose Iyobo ambaye ni dancer wa Diamond Platnumz kubainika kuwa ndio baba kijacho wa mtoto huyo wa staa.
Mbali ya Iyobo pia wapo watu mbalimbali wanahusishwa wakiwemo watu maarufu pia wanasiasa. Modewji Blog tunaweza kusema kimeeleweka kwani hii si mara ya kwanza kwa staa huyo kuachia picha za tumbo lake, kwani kwa upande wa model na video queen, ‘Master snake’ ama mwanadada hodari wa kucheza na nyoka ambaye alipata umaarufu huo wakati wa ushiriki wake wa mashindano ya Ulimbwende nchini, miaka ya nyuma, Hamisa Mabeto ambaye naye licha ya kuficha kwa muda mrefu tumbo lake hilo, mwisho wa siku aliweka wazi na baadae akatupia picha za ‘location’ akiwa amepiga picha huku tumbo lake likiwa wazi, hata hivyo baada ya kuzagaa kwa picha hizo, siku mbili tu akajifungua.
…Kimeeleweka kwa Aunty Ezekiel …tusubiri matokeo ambayo ni dakika 90, ingawa kuna dakika za nyongeza.
Msomaji unayeperuzI mtandao huu endelea kuwa nasi kwa habari motomoto za mastaa, kijamii, matukio na breakingnews!.