Wenyeviti wa serikali za mitaa katika kata ya mikindani manispaa ya Mtwara wamelalamikia manispaa kwa kushindwa kuwapa taarifa mapema kuhusu kuaza kwa zoezi la uandikishwaji kweye daftari la kudumu la wapiga kura hali iliyosababisha wanachi wachache kujitokeza katika vituo vya kujiandikisha.
Wakizungumza na waandishi wa habari baadhi ya wenyeviti hao wamesema zoezi hilo ni nyeti hivyo wananchi wangepaswa kupata taarifa mapema ikiwemo manispaa kutumia magari ya matangazo kipita mitaa mbalimbali ya kata hizo.
Kwa upande wao waendeshaji wa zoezi hilo wamesema ugumu wa kazi unatokana na ugeni wa matumizi ya mashine za BVR vinginevyo zoezi linakwenda vizuri.
Hata hivyo blog hii imeshuhudia katika baadhi ya vituo wananchi wakiwa wachache huku baadhi ya watendaji wa kata hizo wakidai ni siku ya kwanza hivyo muitikio bado ni mdogo na wanaendelea na uhamasishaji, katika kata za mikindani, ufukoni na Mitengo.