Polisi Yamkamata Mtu Mmoja Aliyeingia Kanisani na Bastola Yenye Risasi 8



Hofu‬ imewakumba waumini wa ‪Kanisa‬ ‪Katoliki‬ la Mtakatifu Stephano, ‪‎Kisarawe‬ mkoani ‪‎Pwani‬ katika ibada ya Ijumaa Kuu baada mtu mmoja kukamatwa katikati ya ibada ya Ijumaa Kuu akiwa na bastola yenye risasi nane.

Kwa mujibu wa habari zilizopatikana kutoka kwa waumini na kuthibitishwa na polisi, mwanaume huyo ambaye si muumini wa kanisa hilo anadaiwa kutaka kufanya uhalifu kanisani hapo na alikamatwa baada ya waumini kushtukia mienendo yake isiyo kuwa ya kawaida.

Tukio hili limetokea katika kipindi ambacho kuna tishio la uhalifu unaohusishwa na ‪‎ugaidi‬ katika maeneo mbalimbali nchini, ambapo kuna uporaji wa silaha unaofanywa na watu wasiojulikana baada ya kuwaua polisi.
 
Vilevile tukio hili limetokea wakati waumini hao hawajasahau mauaji ya kutisha nchini ‪Kenya‬ ambako magaidi wamevamia Chuo Kikuu cha ‪‎Garissa‬ na kuua wanafunzi 147.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo