"MCHAWI" APIGWA NA KUTELEKEZWA AKIWA NA MAJERAHA YAKE HUKO GEITA

Mwanamke mmoja aliyejeruhiwa na wananchi ametelekezwa barabarani na wauguzi wa Zahanati ya Nzera iliyopo Geita kwa kile kinachodaiwa ni mchawi.
Hata hivyo kaimu mganga wa Zahanati hiyo Bigaeli Kasala alipinga madai hayo akisema hajatelekezwa bali bali alikuwa akitafutiwa usafiri wa kumpeleka Geita kwa matibabu zaidi.
“Huyu mgonjwa hatujamtupa,niliwakabidhi wahusumu wampandishe basi la asubuhi linalokwenda Geita lakini inaonekana walipitwa na basi hivyo wakamuacha barabarani akisubiri basi jingine”-Kasala.
Dk. Kasala alisema kituo chao hakina gari la wagonjwa ndio maana walimwacha barabarani akisubiri gari lingine.
Awali alidai mwanamke huyo alipelekwa Zahanati hapo wa kituo ch polisi baada ya kumwokoa mikononi mwa wananchi waliokuwa wakimpiga wakimtuhumu kuwa ni mchawi.
Alisema alikutwa kwenye nyumba akiwa mtupu na kutuhumiwa alikuwa akifanya uchawi na ndipo watu wakaanza kumpiga hadi kumvunja kiuno.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo