WAZIRI MKUU PINDA-WAPUUZENI WANAOTUMIA VIBAYA MCHAKATO WA KATIBA MPYA

index
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema kuna baadhi ya watu wamegeuza mchakato wa upatikanaji wa Katiba Mpya kuwa wa kisiasa badala ya kujikita kuwafahamisha wananchi mazuri yaliyomo.
 
 Ametoa kauli hiyo  mwishoni mwa wiki wakati akiwahutubia wakazi wa Kata ya Lwangwa kwenye Halmashauri ya Busokelo wilayani Rungwe akiwa kwenye siku ya nne ya ziara yake mkoani Mbeya kukagua shughuli za maendeleo. “Katiba inayopendekezwa imezingatia maslahi ya kila kundi kwenye jamii hivyo zipuuzeni kauli zinazotolewa na baadhi ya watu kuwa Katiba hiyo haijakidhi malengo ya Kitaifa,” alisema.

 Alisema mabadiliko yaliyofanywa kwenye Katiba hiyo ni asilimia 20, huku asilimia iliyobakia ni sehemu ya mapendekezo yaliyotolewa na Tume ya Jaji Warioba.  Alisema ili kukabiliana na kauli za kiupotoshaji, Serikali imeanza kusambaza nakala za Katiba inayopendekezwa hasa kwenye mikoa ya pembezoni.

 “Jumla ya nakala 300 za Katiba Inayopendekezwa zitasambazwa kwenye kila Kata ambapo makundi yenye uwezo wa kutoa elimu sahihi kuhusiana na Katiba inayopendekezwa yatapatiwa nakala hizo ili kuwaelimisha wananchi,” alisema Waziri Mkuu. 

 Wakati huohuo, akiwa Tukuyu mjini, Waziri Mkuu alizindua ofisi za Halmashauri hiyo baada ya jengo la zamani kupata nyufa kutokana na tetemeko la ardhi. Pia alizindua maabara tatu kwenye shule ya sekondari ya wasichana ya Kayuki.

 Akizungumza na maelfu ya wakazi waliojitokeza kumsikiliza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa michezo wa Tandale jana jioni, Waziri Mkuu aliwataka wakazi hao kujitokeza kwa wingi na kujiandikisha wakazi zoezi la uboreshaji Daftari la Kudumu la Wapiga Kura litakapoanza.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo