MKE AFARIKI DUNIA BAADA YA KUMKUTA MUMEWE AKIMSALITI LAIVU BILA CHENGA

AmbulanceStory ilianza pale ambapo mwanaume aliulizwa na mkewe kama ni kweli ana uhusiano na mwanamke mwingine nje.. mwanaume huyo akakataa, akadai eti ni story za uongo ambazo watu wamezusha.
Emily Nyondo ndio jina la mwanamke huyo toka Zimbabwe, siku ambayo aliona ajihakikishie ukweli alimfuata mume wake ambaye ni Oscar Nyondo nyuma nyuma mpaka kwenye nyumba ya msichana mmoja, mwanaume huyo akaingia ndani halafu akafunga mlango.
Emily hakuridhika, akasogea karibu zaidi mpaka dirishani na kuchungulia ndani ili aone kila kinachoendelea.
Oscar alikuwa kitandani na msichana Mamsie, Emily aliwaangalia na kushindwa kuvumilia kuuangalia usaliti wa mumewe, akaamua kuondoka na kurudi nyumbani.
Baada ya kufika nyumbani alipatwa na mshtuko wa moyo na kuanguka, watu wa huduma ya kwanza walifika kwenye nyumba hiyo na kuthibitisha kuwa mwanamke huyo amefariki kwa ugonjwa wa moyo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo