skip to main |
skip to sidebar
RUFAA YA FRANCIS CHEKA AIBU TUPU....SOMA KILICHOTOKEA
RAIS wa Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO),
Yasin Abdallah ‘Ustaadh’ ameibuka na kufunguka kuwa amevunja kamati yote
iliyokuwa inashughulikia rufaa ya kesi ya bondia wa ngumi za kulipwa,
Francis Cheka ‘SMG’ kwa kuwa wengi wao hawakuwa wakweli.
Cheka, Jana Jumamosi anatimiza siku ya ishirini tangu awe gerezani
kutokana na kifungo cha miaka mitatu baada ya kupatikana na hatia ya
shambulio la kudhuru mwili dhidi ya meneja wa baa yake, Bahati Kibanda,
lililofanyika Julai 2, mwaka jana.
Francis Cheka akiwa kwenye gari la polisi.
Ustaadh alisema imemlazimu kuvunja
kamati hiyo ya watu sita kwa kuwa wengi wao hawakuwa wakweli na
walikuwa wanatafuta umaarufu kupitia jina la bondia huyo.
“Unajua
tulipokuwa Morogoro, tuliunda kamati ambayo ilikuwa na watu sita kwa
ajili ya kushughulikia suala la rufaa ya Cheka lakini nimegundua wengi
wao siyo wakweli na wapo kwa ajili ya kutafuta umaarufu kupitia Cheka,
sasa haitawezekana.
“Kutokana na hali hiyo, nimeunda kamati nyingine mpya inayoongozwa na
mimi mwenyewe akiwemo Juma Msangi, Cosmas Cheka ambao naamini
tutafanikiwa kwa sababu kila kitu kinaenda vizuri kama tulivyotarajia,
kwani ukimya wetu unamaana kubwa sana,” alisema Ustaadh.
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube
Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi