Hawajawahi kukubali hadharani kuwa ni wapenzi lakini picha zinaonesha wazi kuwa mastaa hao wapo kwenye dimbwi zito la mapenzi.
Kupromote wimbo wake mpya ‘Nikuite Nani’, Jux amepost picha akiwa na
hitmaker huyo wa ‘Hawajui’ anayeonekana ‘akimchumu’ kwenye paji la uso.
Kabla ya picha hiyo, Jux alipost nyingine kadhaa akiwa na mrembo huyo katika pozi ambalo huwezi kuuliza kama ni marafiki tu.!
Hivi karibuni Vanessa Mdee alifunguka kuhusu uhusiano wake na
Jux na kusema: "I actually I like to keep my private life private. Nadhani kuna
baadhi ya mambo ambayo hayahitaji majibu.”
Jux na Vanessa wameongozana na Weusi na Navy Kenzo kwenye safari hiyo ya South.