Zaidi ya wanafunzi laki sita wa vyuo vikuu, vyuo vya kati na kidato cha
nne nchini huwenda wasishiriki kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu ujao
kutokana na ratiba ya wizara ya elimu kuhusu mihula ya kufunga na
kufungua vyuo nchini kukinzana ya NEC.
Ratiba
ya mihula ya kufunga na kufungua vyuo ambayo imetolewa na Wizara ya
Elimu mwaka huu, imeibua hofu kwa wasomi wa vyuo mbalimbali nchini
kutoshiriki ipasavyo kwenye uchaguzi mkuu ujao, ambapo jumuiya ya
wanafunzi wa vyuo vikuu ambao ni wanachama wa Chama Cha Demokrasia na
Maendeleo (CHASO) mkoani Mbeya wamelibaini hilo na kuanza kupaza sauti
zao kuidai haki hiyo.
Kutokana na hofu hiyo, CHASO imeandika waraka na kuuelekeza katika ofisi ya katibu mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo ikimtaka kuwatumia wabunge wake kupeleka hoja binafsi bungeni ya kurekebisha sheria ya uchaguzi ili iwaruhusu watanzania wote kupiga kura wakiwa mahali popote ndani ya mipaka ya Tanzania.
Baadhi ya wanafunzi hao pia wameelezea umuhimu wa wao kupiga kura, huku wakidai kuwa hawako tayari kunyimwa haki yao ya kikatiba kwenye uchaguzi mkuu ujao
Kutokana na hofu hiyo, CHASO imeandika waraka na kuuelekeza katika ofisi ya katibu mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo ikimtaka kuwatumia wabunge wake kupeleka hoja binafsi bungeni ya kurekebisha sheria ya uchaguzi ili iwaruhusu watanzania wote kupiga kura wakiwa mahali popote ndani ya mipaka ya Tanzania.
Baadhi ya wanafunzi hao pia wameelezea umuhimu wa wao kupiga kura, huku wakidai kuwa hawako tayari kunyimwa haki yao ya kikatiba kwenye uchaguzi mkuu ujao