MAMA MJAMZITO ASHIKWA NA UCHUNGU KWENYE TRENI, POLISI WALAZIMIKA KUMZALISHA

Katika siku ya christmas watoto wengi walizaliwa katika siku hiyo, lakini mtoto huyu alizaliwa mazingira ambayo wengi walionekana kushangazwa. 

Maafisa wawili wa Polisi Daniel Caban na Darrell James walipewa taarifa ya kutakiwa kutoa msaada wa dharura katika treni ya abiria Philadelphia, walipofika waligundua kwamba dharura yenyewe ni mwanamke ambaye alikuwa katika hali ya kukariba kujifungua, muda haukuruhusu kumkimbiza Hospitali.

Walimsaidia mwanamke huyo kujifungua salama mtoto wa kiume na baadaye wakapelekwa Hospitali ya Hahnemann University wote wakiwa na hali nzuri.

Afisa mmoja amesema alikuwa ameshafungua zawadi zake zote kwa ajili ya siku hiyo na hakujua kama kuna zawadi nyingine ambayo ilikuwa inamsubiria aifungue.

Tukio kama hili liliwahi kutokea mwaka jana baada ya mwanamke mmoja kujifungua mtoto wa kike akiwa kwenye treni ya abiria London lakini yeye alipata bahati ya kusaidiwa na mkunga ambaye alikuwa ndani ya treni hiyo pia.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo