Kikao
cha Bunge la Kenya kilisimama kwa takribani dakika 30 kutokana na
kutofautiana kwa Wabunge hao kuhusiana na msimamo wao kutofautiana
wakati wakiendelea na mjadala unaohusu mabadiliko ya Sheria ya Usalama
wa Nchi hiyo kutokana na kukabiliwa na changamoto mbalimbali kwenye
masuala ya Usalama.
Wabunge wa upinzani walipinga muswada
huo kwa kutupa karatasi chini, Bunge likaahirishwa ambapo hali ya hewa
ilikuwa mbaya na baadaye Wabunge hao kupigana, wengine wakichaniana nguo
na hata kuumizana.
Vikosi vya Usalama vililazimika kulizunguka eneo hilo la Bunge ili kuimarisha Usalama.
Seneta Johnston Muthama alichaniwa nguo na kuumizwa katika vurugu hizo.
Hali ilivyokuwa nje ya Bunge la Kenya leo.
Wabunge wa Upinzani waligomea muswada huo na kuanza kuimba, Bunge hilo likasitishwa.
Nimekurekodia sauti wakati habari hiyo ikiripotiwa na kituo cha WBS unaweza kubonyeza play kuisikiliza, pia kuna video kutoka K24 ambayo unaweza kuitazama hapa.
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube
Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi