WATU 40 WATIWA MBARONI HUKO KATAVI KWA KUNASWA WAKINYWA POMBE SAA ZA KAZI

WAKAZI 40 wa Tarafa ya Inyonga, Makao Makuu ya Wilaya ya Mlele mkoani Katavi wamekamatwa baada ya kukutwa wakinywa pombe asubuhi vilabuni na kwenye maduka yanayouza aina mbalimbali ya vinywaji.
 
Wakazi hao ni pamoja na wanywaji wenyewe na wauzaji wa pombe hizo wakiwemo pia wachezaji wa mchezo wa pool ambapo walikiuka amri ya Mkuu wa Wilaya, Kanali Ngelela Lubinga ya kutocheza pool au kunywa pombe hadi baada ya saa za kazi za ujenzi wa taifa, yaani kuanzia saa 10 jioni.
 
Hivi karibuni, Kanali Lubinga aliamuru wakamatwe baada ya kubainika kukiuka amri yake inayowakataza watu kunywa pombe wala kucheza mchezo wa pool asubuhi.
 
Aliamuru wanamgambo wanaofanya mafunzo wawasake na kuwakamata watu hao na aliiamuru waadhibiwe kwa kuchimba vyoo, kuzibua mitaro na mashimbo ya kutupia taka katika mji huo wa Inyonga kwa siku tatu mfululizo.
 
Kwa mujibu wa Kanali Lubinga operesheni hiyo ni endelevu na yeyote atakayekamatwa akikiuka amri yake hiyo adhabu yake ni kufanya usafi wa mji mzima wa Inyonga.
 
“Tabia hii ya unywaji wa pombe na kucheza pool asubuhi haikubaliki kabisa, lazima watu wajenge tabia ya kujituma kufanya shughuli zao za maendeleo badala ya kuendekeza kunywa pombe na starehe asubuhi,’’ alisisitiza.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo