WAKUNGA WAVAA MIFUKO YA PLASTIKI MAARUFU KAMA RAMBO KUWAZALISHA WAJAWAZITO

Baadhi ya wakunga wa jadi Wilayani Kiteto huvaa mikononi mifuko ya plastiki maarufu kama rambo ili kuwahudumia kina mama wakati wa kujifungua.

Awali wakunga hawa ambao hufanya kazi bila malipo yoyote walikua wakizalisha wajawazito bila kuvaa chochote lakini walianza kutumia aina hiyo ya kinga baada ya wenzao wawili kuambukizwa Ukimwi.

Mmoja wa wakunga hao Rosemary Loshiye alisema walikua wakiwazalisha wakinamama bila kuvaa aina yoyote ya kinga na kusababisha wenzao wawili kuambukizwa Ukimwi kutokana na kuwepo na ukosefu wa vifaa bora kwa ajili ya uzazi.

Alisema wanapouliza sababu za kutopatiwa vifaa vya kuwahudumia wajawazito wanaelezwa kwamba hawatambuliwi na hawapaswi kusaidiwa kuzalisha.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo