Baadhi ya wakunga wa jadi Wilayani Kiteto huvaa mikononi mifuko ya
plastiki maarufu kama rambo ili kuwahudumia kina mama wakati wa
kujifungua.
Awali wakunga hawa ambao hufanya kazi bila malipo yoyote walikua
wakizalisha wajawazito bila kuvaa chochote lakini walianza kutumia aina
hiyo ya kinga baada ya wenzao wawili kuambukizwa Ukimwi.
Mmoja wa wakunga hao Rosemary Loshiye alisema walikua wakiwazalisha
wakinamama bila kuvaa aina yoyote ya kinga na kusababisha wenzao wawili
kuambukizwa Ukimwi kutokana na kuwepo na ukosefu wa vifaa bora kwa ajili
ya uzazi.
Alisema wanapouliza sababu za kutopatiwa vifaa vya kuwahudumia
wajawazito wanaelezwa kwamba hawatambuliwi na hawapaswi kusaidiwa
kuzalisha.