Jeshi la polisi limesitisha mafunzo kwa askari132 waliokua katika
chuo cha Polisi Zanzibar kwa kile kinachodaiwa kuwa ni sababu za kiafya.
Taarifa zilizopatikana kutoka vyanzo mbalimbali vya habari chuoni
hapo kati ya askari hao walioondolewa chuoni hapo mwishoni mwa juma
lililopita mmoja wao Koplo Abdalah alifariki dunia akiwa chumbani
kutokana na shinikizo la damu baada ya kupata taarifa ya kuondolewa
chuoni.
Kamishna wa Polisi Zanzibar Hamdani Makame alisema amewasitishia
kufanya mafunzo kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za kiafya lakini
ajira zao zitaendelea kama kawaida na wataendelea na kazi zao.
Alisema askari aliyefariki alikua akisumbuliwa na kisukari kwa muda
mrefu na alifariki wakati wenzake wakijiandaa kwa mazoezi ya asubui
chuoni hapo.