TAKUKURU YAMFIKISHA MAHAKAMANI MWEKA HAZINA WA JIJI LA MBEYA

Na Keneth Ngelesi wa eddy blog, Mbeya

MWEKAHAZINA Halmashauri ya Jiji la Mbeya, James Jiorojik (59) na Mkurugenzi wa kampuni ya uwakala wa kukusanya ushuru ya (DIEMM) Boniface Magessa (38), jana walipandishwa kizimbani katika Mahakama ya hakimu Mkazi Mbeya kwa makosa ya makosa mnne ya likiwemo kosa la udanganyifu na kujipatia manufaa binafsi kinyume cha sheria.


Kabla ya kufikishwa mahakama na Tasisi Kuzuia na kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) Mkoa wa Mbeya, iliwalikamata watuhumiwa hao,  Oktoba 13 mwaka huu na kushikiliwa katika ya mahabusu ya polisi kutuo cha kati.



Akisoma mashitaka hayo mbele ya hakimu wa mahakama hiyo, Michael Mtaite, Mwendesha mashitaka wa TAKUKURU Mkoa wa Mbeya,Joseph Mulebya, alisema  katika shauri hilo namba 99 la mwaka 2014, washitakiwa kwa pamoja walitenda  makosa hayo kwa lengo la kujinufaisha binafsi.



Mwendesha mashitaka huyo wa TAKUKURU alisema mahakani hapo kuwa,  mshitakiwa namba moja, ambaye ni Mkurugenzi wa kampuni ya (DIEMM), Magessa anahusika na makosa yote manne, ilhali mweka hazina wa Jiji yeye anashitakiwa kwa kosa moja.



Aliyataja makosa hayo kuwa ni udanganyifu, kutoza ushuru wa magari kinyume na taratibu, kuhadaa na kukusanya ushuru kinyume cha sheria, pamoja na kufanya upendeleo kwa lengo la kujipatia manufaa binafsi.



Alisema mbali na kutoza ushuru huo, lakini pia Magesa kupitia kampuni hiyo alikuwa akikusanya ushuru wa magesho katika magari hayo yasiyo ya biashara kinyume kabisa na agizo la mwajiri wake ambaye ni Halmashauri ya Jiji kama ilivyoelekezwa kwenye sheria ndogo za Halmashauri hiyo.



Na kwamba alifanya hivyo , ikiwa ni kinyume cha sheria ya adhabu  namba 304, kifungu cha 16 na marekebisho yake ya mwaka 2002 na ile ya kuzuia na kupambana na rushwa sura ya 11 ya mwaka 2007 .


Wakati shitaka la nne liliwahusu washitakiwa wote wawili la kufanya udanganyifu na upendeleo , ikiwa ni kinyume cha sheria namba 15(i)(a) ya kuzuia na kupambana na rushwa sura ya 11 ya mwaka 2007 .



Washitakiwa  hao wote wanaotetewa na wakili, Ladslaus Rweikaza, walikana mashitaka hayo  wako nje kwa dhamana na  kesi hiyo itaendelea Oktoba 23 mwaka huu.


Hata hivyo, kabla ya kesi hiyo kuanza kusikilizwa ilitawaliwa na vituko, ambapo eddy blog ilishuhudia baada ya watuhumiwa kufikishwa mahakamani hapo, mshitakiwa namba mbili ambaye ni Mwekahazina wa Jiji la Mbeya alionekana kuweweseka.


Mwekahazina huyo aliyeonekana kupagawa alisikika akiwaambia maofisa wa Takukuru waliomfikisha mahakamani hapo wamwache akamalizie kazi zake.


Mweka hazina huyo alikaririwa akisema wamwache kwanza akasaini mafaili, ‘ niacheni nika saini mafaili ….liko wapi lile faili na zile LPO,, hali iliyoibua vicheko kwa watumishi wenzake waliokuja kumpa pole na kusikiliza kinachooendelea.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo