Wanafunzi wawili wa darasa la pili wenye miaka saba na mwingine nane
wa Shule ya Msingi Kikunku Kigoma wameadhibiwa na walimu wao kutokana
na tabia yao ya kufanya mapenzi katika umri mdogo na kusababisha walimu
watatu kushikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumjeruhi mtoto wa kiume.
Akizungumzia tukio hilo mwalimu mmoja wa shule hiyo Nicholous
Ulimwengu alisema wazazi wa watoto hao walilamika wanafunzi hao kila
siku kuchelewa kurudi nyumbani na kuamua kufuatilia shuleni hali
iliyowafanya walimu kuchunguza na kugundua huwa mara baada ya masomo
kuenda sehemu ya kujificha na kufanya tendo hilo.
Alisema baada ya kugundua tabia za wanafunzi hao walimu waliamua
kuwaadhibu kwa kuwachapa viboko vinne kila mmoja ambapo mzazi wa mtoto
wa kiume aliamua kwenda kushtaki polisi baada ya mwanae kulalamika
kupata majeraha ndipo polisi wakaamua kuwashikilia walimua hao kutokana
na adhabu hiyo wakati uchunguzi ukiendelea.