Mwanariadha wa Afrika Kusini, Oscar Pistorius akiwa mahakamani siku ya leo.
Aimee
Pistorius (katikati) akimuangalia kaka yake, Oscar Pistorius wakati
wakili wake Barry Roux's akiendelea kumtetea (hayupo pichani), Kulia wa
pili ni shangazi yake, Lois akiwa na mjomba wake Arnold (kulia).
Oscar Pistorius akilia baada ya wakili wake kusema kuwa pesa zake zimekwisha baada ya kesi yake kuendeshwa kwa miezi saba.
Mahakama inayosikiliza kesi dhidi ya mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini, Oscar Pistorius imeambiwa kuwa mwanariadha huyo amefilisika. Pistorius alipatikana na hatia ya mauji ya mpenzi wake Reeva Steenkamp bila ya kukusudia mwaka jana.
Jaji Thokozile Masipa anatarajiwa kutoa hukumu dhidi ya Pistorius
Jumanne. Anakabiliwa na kifungo cha miaka 15 lakini jaji anaweza kuamua
kumpa kifungo cha nje au hata kumtoza faini.
Upande wa mashitaka unataka Pistorius apewe adhabu kubwa kuambatana na kosa lake.
Pistorius aliangua kilio wakili wake alipoambia mahakama kuwa amefilisika
Pistorius aliangua kilio wakili wake aliposema kuwa pesa zake zimekwisha baada ya kesi yake kufanya kwa miezi saba.
"sio tu kwamba hana pesa bali anahisi hana tena matumaini,'' alisema wakili wa Pistorius.
(HABARI NA MTANDAO)