Abiria zaidi ya abiria 30 wamejeruhiwa vibaya baada ya basi Mwafrika walilokuwa wakisafiria kutoka wilayani Makete mkoani Njombe kweda mkoani Iringa kuacha barabara na kuingia kwenye ukingo wa barabara wakati akikwepa kugongana uso kwa uso na basi la Super Feo
Kwa mujibu wa shuhuda aliyekuwepo eneo la tukio Bw. Linus Matofali amemwambia mwandishi wa eddy blog Riziki Manfred kuwa chanzo cha ajali hiyo ni basi la Super Feo kulipita trekta lililokuwa mbele yake bila kuchukua tahadhari na ghafla walikutana barabarani na katika harakati za dereva wa basi la Mwafrika kukwepa kugongana uso kwa uso alihama barabara na kupelekea kuingia ukingonina kisha kubinuka
Ajali hiyo imetokea hii leo majira ya saa nne asubuhi eneo la Kibena nje kidogo ya mji wa Njombe ikilihusisha basi hilo lenye namba za usajili T 726 AGA
Mganga mfawidhi wa hospitali ya Kibena Dkt. Patrick Msigwa ameieleza eddy blog kuwa hospitali yake imepokea majeruhi 32 ambapo miongoni mwao wanaume ni 15 na wanawake 17 ambao mpaka tunaandika habari hii majina yao hayakufahamika mara moja
Muonekano wa basi hilo.
Dkt Msigwa amesema mmoja wa majeruhi hao Bi. Jane Chengula mwenyeji wa kijiji cha Makangalawe wilayani Makete alionekana kujeruhiwa zaidi kwa kuvunjika mkono wake mara mbili hivyo anaendelea na matibabu hospitalini hapo na majeruhi wengine wamepatiwa matibabu na kuruhusiwa lakini wengine wamepelekwa hospitali ya Consolatha Ikonda kwa matibabu zaidi
Aidha mwandishi wetu amesema basi hilo la Mwafrika limeharibika zaidi upande wa kushoto kwa kubondeka na kupasuka vioo
Kamanda wa polisi mkoani Njombe SACP Fulgence Ngonyani amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa dereva wa basi hilo Bw. Furaha Sanga anashikiliwa kwa mahojiano zaidi
Amesema bado chanzo cha ajali hiyo hakijafahamika mpaka sasa kwa kuwa wanaendelea kumuhoji dereva pamoja na mashahidi wengine ili kubaini chanzo cha ajali hiyo
Kamanda Ngonyani ametoa wito kwa madareva kufuata sheria za barabarani ikiwemo alama zilizopo ili kuepusha ajali kwa kuwa zinaelekeza hali ya barabara ilivyo
Kamanda wa polisi mkoani Njombe SACP Fulgence Ngonyani amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa dereva wa basi hilo Bw. Furaha Sanga anashikiliwa kwa mahojiano zaidi
Amesema bado chanzo cha ajali hiyo hakijafahamika mpaka sasa kwa kuwa wanaendelea kumuhoji dereva pamoja na mashahidi wengine ili kubaini chanzo cha ajali hiyo
Kamanda Ngonyani ametoa wito kwa madareva kufuata sheria za barabarani ikiwemo alama zilizopo ili kuepusha ajali kwa kuwa zinaelekeza hali ya barabara ilivyo
Habari/picha na Riziki Manfred Bonzuma, Eddy Blog