MNYIKA ACHUKUA CHEO CHA ZITTO KABWE NDANI YA CHADEMA


MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Taifa, Freeman Mbowe amewateua Dk. Willbrod Slaa kuwa Katibu Mkuu, John Mnyika kuwa Naibu Katibu Mkuu Bara na Salum Mwalim ambaye anakuwa Naibu Katibu Mkuu Zanzibar. 
 
Viongozi hao wameteuliwa jana usiku na kupitishwa na Baraza Kuu la Chadema hivyo kufikia tamati ya uchaguzi wa ndani ya chama hicho.
 
Mhe. John Mnyika anateuliwa kushika nafasi ambayo ilikuwa inashikiliwa na Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Mhe. Zitto Kabwe ambaye aliondolewa katika nafasi hiyo na kamati kuu ya chama hicho kwa kudaiwa kuvunja katiba ya chama.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo