MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Taifa,
Freeman Mbowe amewateua Dk. Willbrod Slaa kuwa Katibu Mkuu, John Mnyika
kuwa Naibu Katibu Mkuu Bara na Salum Mwalim ambaye anakuwa Naibu Katibu
Mkuu Zanzibar.
Viongozi hao wameteuliwa jana usiku na kupitishwa na Baraza Kuu la Chadema hivyo kufikia tamati ya uchaguzi wa ndani ya chama hicho.
Viongozi hao wameteuliwa jana usiku na kupitishwa na Baraza Kuu la Chadema hivyo kufikia tamati ya uchaguzi wa ndani ya chama hicho.
Mhe. John Mnyika anateuliwa kushika nafasi ambayo ilikuwa
inashikiliwa na Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Mhe. Zitto Kabwe
ambaye aliondolewa katika nafasi hiyo na kamati kuu ya chama hicho kwa
kudaiwa kuvunja katiba ya chama.
