UKAWA WAZIDI KUSISITIZA KUWA HAWATARUDI BUNGENI, WAWEKA MASHARTI YAO




Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA),umesema  umesikitishwa na kauli za baadhi ya viongozi wa dini zilizotolewa wakati wa baraza la Iddi za kuwataka warejee katika bunge maalum la katiba huku viongozi hao wakinyamaza bila ya kukemea matendo yaliyosababisha wajumbe wa umoja huo  kususia vikao vya bunge hilo.
 
Akizungumza kwa niaba ya wajumbe wa umoja huo, Mwenyekiti wa chama cha wananchi-CUF, Prof. Ibrahim Lipumba,  amesema UKAWA  wanatambua kuwa viongozi wa dini ni watu wenye heshima na nafasi ya pekee katika jamii, hivyo wana kila sababu ya kuheshimu miito na ushauri wao.
 
Prof. Lipumba aliyasema hayo jana  jijini Dar e s salaam wakati viongozi wa UKAWA walipokutana kwa ajili ya kutoa tamko kuhusu miito ya viongozi wa dini kuwataka kurejea kwenye  bunge maalum la katiba Jumanne ijayo.
 
Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA Freeman  Mbowe alisema kuwa anasikitika kuona kauli za viongozi mbalimbali wa CCM pamoja na Serikali wakitoa matamko ambayo hayaashirii kutafuta muafaka.
 
Aidha Mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi Jemes  Mbatia alisema ipo haja ya serikali kuangalia namna ya kuboresha sheria ya uchaguzi ili kutoa nafasi ya kufanyika kwa uchaguzi mwakani kutokana na dalili zilizopo ni dhahiri kuwa katiba mpya haiwezi kupatikana katika kipindi kilichopangwa.
 
UKAWA wamedai kuwa   waliamua kuondoka bungeni ili kupinga njama zilizokuwa zikifanywa na wajumbe wa chama cha Mapinduzi za kuhujumu mchakato wa katiba mpya, kupinga kauli za kejeli, lugha za ubaguzi, uchochezi  na matusi, pamoja na kile walichosema ni kushindwa kwa mwenyekiti wa Bunge hilo kuwadhibiti wajumbe wanaokiuka kanuni


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo