Utangulizi
Ndugu wananchi;
Naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema, kwa kutujalia uzima na kutuwezesha kwa mara nyingine tena kuzungumza na taifa juu ya masuala muhimu yanayohusu nchi yetu. Mwezi wa Saba tunaoumaliza leo ulikuwa na matukio mengi baadhi yakiwa makubwa na kushtusha na mengine yalikuwa matukio ya kawaida.
Mashambulio ya Mabomu
Ndugu Wananchi;
Tarehe 3 Julai, 2014 na tarehe 07 Julai, 2014 kulitokea mashambulizi ya mabomu nyumbani kwa Sheikh Sudi Ally Sudi na katika mgahawa wa Vama kwa mfuatano huo. Kabla ya hapo, kulikuwa na matukio mengine matatu: Kanisa la Olasiti tarehe 5 Mei, 2012, Mkutano wa Kampeni wa CHADEMA tarehe 15 Juni, 2013 na Baa ya Arusha Night Park tarehe 13 Aprili, 2014. Hali kadhalika, tarehe 13 Juni, 2014 kulitokea shambulizi la mabomu katika eneo la Darajani, Zanzibar.
Ndugu Wananchi;
Tarehe 3 Julai, 2014 na tarehe 07 Julai, 2014 kulitokea mashambulizi ya mabomu nyumbani kwa Sheikh Sudi Ally Sudi na katika mgahawa wa Vama kwa mfuatano huo. Kabla ya hapo, kulikuwa na matukio mengine matatu: Kanisa la Olasiti tarehe 5 Mei, 2012, Mkutano wa Kampeni wa CHADEMA tarehe 15 Juni, 2013 na Baa ya Arusha Night Park tarehe 13 Aprili, 2014. Hali kadhalika, tarehe 13 Juni, 2014 kulitokea shambulizi la mabomu katika eneo la Darajani, Zanzibar.
Kila
lilipotokea shambulizi uchunguzi ulifanyika na watuhumiwa kukamatwa.
Lakini, watuhumiwa waliokamatwa safari hii wanaelekea kutoa sura nzuri
zaidi ya mtandao wa watu wanaofanya vitendo hivi vya kikatili pale
Arusha na kwingineko nchini. Watu 38 wameishafikishwa Mahakamani, wengine 8 watafikishwa Mahakamani kesho na uchunguzi na msako unaendelea kote nchini kuwapata watuhumiwa wengine.
Napenda
kutumia nafasi hii kutoa pongezi za dhati kwa vyombo vyetu vya ulinzi
na usalama kwa kazi kubwa na nzuri iliyotufikisha hapa tulipo sasa.
Tunawaomba waongeze bidii, maarifa na ushirikiano mpaka wote waliohusika
wakamatwe na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Aidha,
natoa pongezi na shukrani maalum kwa wananchi wema waliotoa taarifa
zilizowezesha kukamatwa kwa watuhumiwa. Napenda kutumia nafasi hii
kuwasihi wananchi wenye taarifa kuhusu wanaotafutwa au ye yote
anayejihusisha na vitendo hivi viovu watoe taarifa kwenye vyombo vya
usalama ili hatua zipasazo zichukuliwe.