Mtoto Rebecca James ambaye ni mlemavu wa miguu na aliyekuwa haongei, ameteketea hadi kufa baada ya nyumba yao kuwaka moto.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura alisema moto huo ulizuka
ghafla juzi huko Magomeni Kagera kwenye nyumba hiyo inayomilikiwa na
Rashid Khalfani (64), mkazi wa Magomeni.
Alisema moto huo uliteketeza chumba cha kulala cha binti huyo na ulimuunguza hadi kufa akiwa ndani ya chumba hicho.
Alisema
kwa mujibu wa mama wa watoto hao, Bahati Karuti aliwaacha watoto hao
peke yao na kwenda kwenye shughuli zake za kuuza mkaa.
