Mtoto Mlemavu wa Miguu ateketea kwa moto hadi kufa baada ya nyumba yao kuungua Moto



Mtoto Rebecca James ambaye ni mlemavu wa miguu na aliyekuwa haongei, ameteketea  hadi kufa baada ya nyumba yao kuwaka moto. 
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura alisema moto huo ulizuka ghafla juzi huko Magomeni Kagera kwenye nyumba hiyo inayomilikiwa na Rashid Khalfani (64), mkazi wa Magomeni. 
 
Alisema moto huo uliteketeza chumba cha kulala cha binti huyo na ulimuunguza hadi kufa akiwa ndani ya chumba hicho.
 
Alisema kwa mujibu wa mama wa watoto hao, Bahati Karuti aliwaacha watoto hao peke yao na kwenda kwenye shughuli zake za kuuza mkaa.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo