MSANII BATULI ADAI YUPO TAYARI KUACHANA NA KUIGIZA FILAMU ENDAPO.....!!!!



BATULI  amesema  kuwa  anahitaji  kwenda  kusomea  uhudumu  wa  ndege  lakini  anashindwa  kufanya  hivyo  kwa  sababu  ya  kubanwa  na  maisha, lakini  endapo  atapata  mtu  wa  kumlipia  ada  yupo  tayari  kuachana  na  filamu  na  kwenda  kusoma.

Mrembo  huyo  akizungumza  na  mwandishi  hivi  karibuni  aliweka  wazi  ishu  hiyo  kwa  madai  kwamba  anahitaji  kutimiza  ndoto  yake  juu  ya  suala  hilo  kwani  ni  wazo  lake  la  muda  mrefu  ingawa  hakuwahi  kumwambia  mtu  yeyote....

"Napenda  sana  kazi  hiyo  ikibidi  hata  urubani  kabisa  pia  naona  naweza  kufanya.Tatizo  ni  gharama, naamini  endapo  ntapata  mtu  wa  kunidhamini  naweza  kwenda  kusomea  ili  nitimize  ndoto  zangu  za  muda  mrefu,"alisema


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo