CHADEMA MBEYA KUJA NA BANDIKA BANDUA YA KUIMARISHA CHAMA NGAZI YA MITAA

Mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na Maendeleo  (Chadema) Mbeya mjiji John Mwambigija “Mzee wa Upako” akiwahutubia wananchi wa Kata ya Manga jiji Mbeya, wakati wa ziara ya Mbunge wa Jimbo hilo Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ katika zira ya kutoa taarifa ya utekeleza wa ahadi alizo toa mwaka 2010 wakati akiomba ridhaa ya kuwa Mbunge (Picha na Kenneth Ngelesi)
Mbunge wa Mbeya mjini  Joseph Mbilinyi akiwa hutubia wananchi wa Mtaa wa Mafiat kata ya Manga jiji Mbeya katika Mkutano wa hadara ambo ni kwa ajili ya kuto taafifa za utekelezaji wa ahadi alizotoa  mwaka 2010 wakati akiomba ridhaa ya kuwa Mbunge

NA KENNETH NGELESI,MBEYA

SIKU  chache baada ya kupata viongozi wapya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),Mkoani hapa kimesema kimejipanga kufanya mikutano kila kata kwa ajili ya kutoa elimu ya Uchuguzi wa Serikali za mitaa unao tarajia kufanbyika Oktoba Mwaka huu.

Chama hicho kimekusudia kumbana na chama cha Mapinduzi ili kujihakikishia ushindi wa kishindo  na kuweza kukibura chama cha Mapinduzi CCM katika uchaguzi huyo.

Akiwahutubia wananchi jana na Mwenyekiti wa chama hicho, Wilaya ya Mbeya Mjini, John Mwambigija, katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Nsalala, Mjini Mbalizi,alisema kuwa mikutano hiyo itakayofanyika kila kata na kwamba imepewa jina la  bandika bandua.

Mwenyekiti huyo ambaye ametetea nafai hiyo katika uchaguzi ulio fanyika Agost mwaka huu alisema chama hicho, mkoa wa Mbeya licha ya kutumia mikutano hiyo kuwajengea uwezo wananchi kabla hawajafikia hatua ya kufanya maamuzi ya kuwachagua viongozi wao wa serikali za mitaa katika uchaguzi wa Oktoba, lakini pia inalenga kukiimarisha chama hicho ngazi za chini.

Mwambigija alisema wananchi katika ngazi za mitaa, vitongoji na kata wanafursa ya kujua umuhimu wa kuchagua viongozi bora, wataoweza kuwawezesha kupata maendeleo wanayoyatarajia badala ya kuendelea kulalamika.

Katika mkutano huo uliokusanya mamia ya wananchi wa kata hiyo ya Nsalala, jumla ya wanachama 15 kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM) walirudisha kadi na kukabidhiwa kadi mpya za chadema.

Wakati wanachama hao 15 wakirudisha fomu za CCM, chama hicho cha Chadema kilifanikiwa kuvuna wanachama wapya 71 waliochukua fomu na kula kiapo cha kuwa wanachama.

Viongozi mbalimbali wa Chadema, akiwemo Mbunge wa jimbo la Mbeya, Mjini Joseph Mbilinyi (Sugu), ambaye na ameungana na wenzake wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kugomea bunge la katiba , ameungana na viongozi wake wa mkoa kuendesha mikutano hiyo ya bandika bandua katika kata mbalimbali mkoani Mbeya.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo