DIAMOND ATANGAZA KUACHIA VIDEO MBILI KWA MPIGO, ADAI ZITAKUWA TOFAUTI NA ZOTE ALIZOWAHI KUFANYA



Diamond Platinumz ametangaza kupitia Instagram kuwa ataachia video mbili kwa mpigo ikiwa ni siku chache baada ya kumalizana na BET Awards 2014.
 
Mashabiki wake wategemee kuona video mbili kwa wakati mmoja ambazo ni moja ya wimbo aliofanya na mkali wa Kukere, Iyanya wa Nigeria, na nyingine ya wimbo wenye asili ya ngoma za kitanzania Kitorondo aliyoipa jina la MdogoMdogo.
 
Diamond ameendelea kushare picha mbalimbali kutoka kwenye video hizo, picha zinazoashiria kuwa video hizo zitakuwa tofauti kabisa na video za awali za Diamond.
 
Katika moja ya picha alizoshare Instagram akiwa katika eneo lenye miamba na maporomoko ya maji huku akiwa amevaa kama mtu anaeishi nyikani, aliwataka mashabiki wataje uhusika wake.
 
“Nikikupa Nafasi moja tu ya Kunipa Jina katika Caracter hiyo we ungenipa jina Gani?..... [ If I was to give you a chance to give me a name from that character what would it be...?]”

Hata hivyo, bado hajatangaza tarehe rasmi atayoziachia video hizo na amewataka mashabiki kupendekeza tarehe.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo