TUKIO LA AJABU LINALOHUSISHWA NA USHIRIKINA KAZINI, LATOKEA LEGHO SINZA!

Mwathirika akisugua miguu chini kama vile anawashwa na vitu mwilini.
 
MTU mmoja ambaye anasadikiwa kula chakula na baadaye kuanza kuchanganyikiwa alinaswa na kamera yetu leo akisugua miguu ardhini na kujikuna mwili mzima, jambo ambalo lilidaiwa na wapita njia kuwa alikuwa amekula chakula kilichokuwa maalumu kwa ajili ya kafara.  

Haikujulikana chakula hicho amekila wapi na ni chakula gani.  Jina lake pia halikuweza kupatikana mpaka kamera yetu inaondoka sehemu hiyo.

Tukio zima limetokea eneo la  Sinza-Legho Mtaa wa Shekilango, jijini Dar es Salaam,  kwenye kampuni ya magari makubwa ya usafirishaji.

(Picha na Gabriel Ng’osha/GPL)


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo