MTOTO AFARIKI DUNIA BAADA YA KUTUMBUKIA KISIMANI


Mtoto Jeremiah Nyamuhanga (2) mkazi wa Machimbo amekufa baada ya kutumbukia kwenye kisima cha maji karibu na nyumbani kwao.
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Marietha Minangi alisema, mtoto huyo alitumbukia juzi saa 10 jioni katika eneo la Machimbo, Kitunda, Wilaya ya Ilala.
 
Alisema maiti yake ilikutwa ikielea ndani ya kisima hicho kilicho karibu na nyumba yao. Inasadikiwa mtoto huyo alimtoroka baba yake aliyekuwa kwenye banda la kuku na kwenda kucheza ambapo alitumbukia ndani ya kisima hicho.
 
Maiti ya mtoto huyo amehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na upelelezi unaendelea.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo