Kijana mmoja aliyetambulika kwa jina moja la sule amenusurika kifo baada ya kupigwa na watu wenye hasira kali wakimtuhumu kuwa ni mwizi jambo ambalo baadaye lilikuja kubainika kuwa hana hatia yoyote.
Wakizungumza eneo la feri jijini Dar es salaam
baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo wamesema kuwa inasikitisha kuona watu
wakijichukulia sheria mikononi bila kuhoji tukio ambapo mara baada ya
kipigo ambacho kimemsababishia majeraha makubwa kijana huyo hakuna mtu
aliyejitokeza kulalamika kuibiwa wala kujulikana kijana huyo ameiba
nini.
Akiongea kwa shida kijana huyo amesema kuwa yeye hakuiba chocho na hajui kwa nini watu walimvamia na kuanza kumpiga
Akiongea kwa shida kijana huyo amesema kuwa yeye hakuiba chocho na hajui kwa nini watu walimvamia na kuanza kumpiga
Katika hatua nyingine ya kujaribu kunusuru maisha
ya kijana huyo baadhi ya wasamalia wema waliamua kumfikisha kijana huyo
katika vyombo vya usalama lakini mara baada ya kumfikisha katika kituo
kidogo kilichopo karibu na hapo walikuta kituo hicho kimefungwa na
kufuri na hakuna askali yoyote lakina baada ya muda askali polisi mmoja
alitokea..
Bonyeza hapo chini kuona video ya tukio hilo
CHANZO:ITV
Bonyeza hapo chini kuona video ya tukio hilo

