skip to main |
skip to sidebar
KENYA YASHAMBULIWA TENA, WATU WATANO WAPOTEZA MAISHA USIKU WA KUAMKIA LEO
WATU
watano wamepoteza maisha baada ya shambulio lililotokea usiku wa
kuamkia leo katika kijiji cha Pandanguo huko Witu wilayani Lamu nchini
Kenya kilometa 30 kutoka Mpeketoni yalipotokea mauaji ya watu zaidi ya
60 wiki iliyopita.
Polisi wamesema kuwa waliouawa ni kutoka jamii mbalimbali.
Mkuu wa
Polisi nchini Kenya, David Kimaiyo amesema kuwa washambuliaji walivamia
kijiji cha Pandanguo na kuua takribani watu watano.
"Bado tunawasaka waliohusika na shambulio hili, habari zaidi zitatolewa baadaye," alisema Kimaiyo.
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube
Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi