Wakazi hao wametoa malalamiko hayo wakati wakiongea Juni
13, 2014 na kusema wamekuwa wakidaiwa kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili
ya kupatiwa huduma husika na baadhi ya watoa huduma za afya mkoani
humo, na pindi wanaposhindwa kutoa fedha kidogo ‘rushwa’ wagonjwa wao
hukosa huduma kwa muda mrefu na kuendelea kubaki hospitalini, zahanati
na katika vituo vya afya kwa muda mrefu.
Kaimu Mkuu wa mkoa wa Ruvuma ambaye
pia ni Mkuu wa Wilaya ya Songea, Joseph Mkirikiti, ameahidi
kushughulikia kero hizo ya huduma ya afya pamoja na malalamiko mengine
ya wananchi ambayo ameyapata likiwemo suala la mahusiano mabaya baina ya
wananchi na Jeshi la Polisi mkoani humo.
Amekemea na kupiga marufuku tabia ya
viongozi wa siasa wilayani humo, kutumia nafasi ya kuwarubuni wananchi
kwa changamoto zinazowakabili katika kipindi cha uchaguzi wa serikali za
mitaa unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni, kwani kufanya hivyo upo
uwezekano wa kuchochea vurugu na machafuko kwa wananchi kudai haki zao
kwa nguvu.
licha ya Mganga Mkuu Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa mkoani humo,
Benedicto Ngaiza, kuwataka wananchi kutokubali kutoa rushwa kwa ajili ya
huduma yoyote na pindi wanapodaiwa rushwa watoe taarifa kwa uongozi
wowote ili hatua ziweze kuchukuliwa dhidi ya wahusika bado tatizo hilo
limeendelea kuota mbawa.
CHANZO:FIKRA PEVU