Ndugu Wananchi,
Tuna wajibu mkubwa wa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutupa afya na uzima tukaweza kujumuika leo hii. Napenda kutoa shukurani zangu za dhati kwa viongozi wa Kanisa la Anglikana wa Dayosisi ya Zanzibar na waumini wote wa Kanisa hili kwa kunialika kuja kuungana nanyi katika uzinduzi wa kongamano la kumuenzi Dk. David Livingstone kwa kutambua mchango wake katika kukomesha biashara ya utumwa.
Napenda kutoa pongezi kwa maandalizi mazuri ya kongamano hili pamoja na uteuzi mzuri wa mada ambazo zimeandaliwa kuwasilishwa na baadae kuchangiwa na washiriki wa kongamano hili.
Nawapongeza wahadhiri wote waliochaguliwa
kuwasilisha mada katika kongamano hili kwa heshima kubwa waliyopewa.
Kadhalika, napenda kuchukua fursa hii kuwakaribisha wageni wetu wote
waliotoka nje ya Zanzibar kuja kushiriki kwenye Kongamano hili. Wote
nawashauri watumie fursa hii kutembelea na kuona maeneo mbali mbali ya
kihistoria na utajiri wa maumbile ambao Mwenyezi Mungu ameitunukia
Zanzibar.
Ndugu Viongozi na Ndugu Wananchi,
Sote tuna wajibu wa kuwapongeza marafiki wa Dk. David Livingstone (FDDL) kwa kubuni utaratibu huu wa kufanya maadhimisho ya miaka 141 tangu kukomeshwa kwa biashara ya utumwa hapa Zanzibar.
Ndugu Viongozi na Ndugu Wananchi,
Sote tuna wajibu wa kuwapongeza marafiki wa Dk. David Livingstone (FDDL) kwa kubuni utaratibu huu wa kufanya maadhimisho ya miaka 141 tangu kukomeshwa kwa biashara ya utumwa hapa Zanzibar.
Vitabu vya historia
vinaeleza kuwa Soko Kuu la Watumwa la Afrika ya Mashariki lililokuwepo
hapa Zanzibar, lilifungwa rasmi tarehe 06 Juni (tarehe ya leo) mwaka
1873. Hatua hiyo ina mchango muhimu unaotokana na wamishionari wa
madhehebu ya UMCA pamoja na juhudi za Dk. David Livingstone.
Nimefurahi kusikia kuwa utaratibu huu wa kufanya maadhimisho haya kila mwaka ni wa kupokezana ambapo mwaka jana; 2013 ilikuwa ni zamu ya wenzetu wa Bagamoyo na mwaka huu wa 2014 ni zamu ya Zanzibar.
Nimefurahi kusikia kuwa utaratibu huu wa kufanya maadhimisho haya kila mwaka ni wa kupokezana ambapo mwaka jana; 2013 ilikuwa ni zamu ya wenzetu wa Bagamoyo na mwaka huu wa 2014 ni zamu ya Zanzibar.
Hali hii
inadhihirisha kuwepo kwa uhusiano mkubwa wa kihistoria baina ya wananchi
wa Tanzania Bara yakiwemo maeneo ya mwambao kama vile Bagamoyo.
Vile
vile, hali hii ni kutokana na nafasi ya Zanzibar kuwa ni kitovu cha
ziara za wageni wengi kupitia hapa katika ziara zao za maeneo mbali
mbali ya Afrika Mashariki na Kati kama ilivyokuwa kwa Mmishionari huyo,
Dk. David Livingstone aliyepita Zanzibar kati ya mwaka 1853 na 1856.
<<BONYEZA HAPA KUENDELEA KUISOMA>>
Hotuba ni Ndefu, Ingia hapo juu kuendelea nayo .
<<BONYEZA HAPA KUENDELEA KUISOMA>>
Hotuba ni Ndefu, Ingia hapo juu kuendelea nayo .
