BABY MADAHA AFUGUKA, "SIAMINI KAMA ADAM KUAMBIANA NA RECHO WAMEKUFA MPAKA NIONE MAKABURI"

MSANII wa filamu na muziki Bongo, Baby Joseph Madaha (pichani juu) ambaye kwa sasa yuko Kenya amesema kuwa, haamini kama kweli wasanii wa filamu Recho Haule na Adam Kuambiana wamefariki dunia mpaka siku atakapoyaona makaburi yao.

Maziko ya Msanii Recho yaliyofanyika katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar.

Akizungumza na Ijumaa kwa njia ya simu, Madaha alisema ameshitushwa na vifo hivyo na vimemfanya akose amani kutokana na namna walivyoondoka duniani ghafla.
 Jeneza lenye mwili wa marehemu Adam Kuambiana.

“Nilitamani sana kuwepo lakini niko mpakani mwa Kenya na Uganda kuna ziara maalum ya kikazi naifanya.

Yaani bado siamini kama kweli wamefariki, mpaka nije nione walipozikwa,” alisema Baby Madaha.

>>>>GPL


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo