Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa kata ya
Ufuluma wilaya ya Uyui ambapo aliwaambia wananchi hao Kilimo cha
Tumbaku kiondoe umasikini na si kuongeza umasikini kwa mkulima.
Wakulima
wa Tumbaku kata ya Ufuluma wamelalamikia kulazimishwa na viongozi wa
vyama vya ushirika kuuza tumbaku yao katika vyama hivyo ,hata kama sio
wanachama.Kinana amewataka wakulima hao kutokukubali kusumbuliwa kuuza
tumbaku yao katika vyama hivyo ambavyo baadhi yake vimejaa walaghai na
wanyonyaji wa wakulima hao.
Amesema
kuwa Wakulima wa zao hilo la tumbaku wamekuwa wakifanya kazi kubwa na
ngumu,lakini hawafaidika na jasho la kazi yao,kutokana na kuanzishwa kwa
vyama vingi vya ushirika ambavyo vipo kwa faida ya wajanja
wachache,hivyo wakulima hao wasilazimishwe kuuza tumbaku yao kwa vyama
vya ushirika.
Nae
Mkuu wa Mkoa wa Tabora,Mh Fatma Mwasa aliongeza kuwa mnamo mwaka 2012
wakulima wa Tumbaku waliibiwa kiasi cha fedha shilingi Bilioni 16,kama
vile haitoshi mnamo mwaka 2013 wakulima hao waliibiwa kiasi cha fedha
shilingi bilioni 12 na umoja wa vyama vya ushirika,akabainisha kuwa
kufuatia ubadhilifu huo mkubwa wa fedha kwa wakulima,mwaka huu tumbaku
haitatolewa kienyeji kwa vyama hivyo mpaka wahakikishiwe fedha zao
zitalipwaje.
Akabainisha
kuwa imefika wakati wakulima wa Tumbaku wajitegee,wawe huru na kuamua
ni wapi wauze tumbaku yao na kwa bei waitakayo ni si kupangiwa na vyama
vya ushirika,akaongeza kwa kusema kuwa Wakulima hao wasilazimishwe kuuza
tumbaku yao kwa Vyama vya ushirika.
Kinana amemaliza ziara yake wilayani Uyui leo na kesho ataunguruma wilayani Sikonge mkoani Tabora.
Wakazi
wa Ufuluma wakishangilia na wengine wakifuatilia jambo kwenye mkutano
uliofanyika leo kwenye kata hiyo ya Ufuluma,wilayani Uyui mkoani
Tabora.


