MWANAFUNZI WA MIAKA 11 AFARIKI PAPO HAPO BAADA YA KUGONGWA NA GARI MKOANI MBEYA

Mwanafunzi wa shule ya msingi Jangurutu darasa la tano aliyetambulika kwa jina la Habibu Dismass (11) amefariki dunia papo hapo baada ya kugongwa na gari lenye namba za usajili T.120 AMV aina ya Camry lililokuwa likiendeshwa na derava Otino Mwampamba (48) mwalimu shule ya sekondari, Mbarali. 

Tukio hilo limetokea jana majira ya saa 10:15 jioni huko katika kijiji cha Mabanda, kata na tarafa ya Rujewa wilaya ya Mbarali mkoa wa Mbeya. Chanzo cha ajali ni mwendo kasi. Dereva amekamatwa na gari lipo polisi-Rujewa. 
 
Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya kamishina msaidizi mwandamizi wa polisi Ahmed Msangi anatoa wito kwa madereva kuwa makini wanapotumia vyombo vya moto hasa kwa kuzingatia sheria na alama za usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika. 
 
Aidha anatoa wito kwa watembea kwa miguu kutembea pembeni mwa barabara na kuvuka sehemu zenye vivuko ili kuepuka ajali.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo