Ugonjwa wa kuvuja kwa nyimbo ambazo hazijakamilika au muda wake wa
kutoka haujafika umemkuta tena mshindi wa tuzo saba za KTMA, Diamond
Platnumz.
Wimbo huo uliopewa jina la "Kitorondo" umesambaa jana katika
baadhi ya blogs pamoja na mitandao ya kijamii.
Platnumz ametoa kauli kuhusiana na wimbo huo: "Moja ya nyimbo zangu ambazo ziko "store" hazija toka nimeikuta mtandaoni
na sijui imefikaje, tena ikiwa kwenye mfumo wa Voicenote, yaani haina
quality kabisa" Tafadhari, kwa yoyote atakayeipata Asiitumie kwenye
media ama hadhara, kwa sababu Haijatoka na haiko Qualified.
