Taarifa
ambazo zimetufikia leo hii ni kwamba mtangazaji maarufu wa radio one na
ITV Reuben Mchome ameacha kazi rasmi katika vituo hivyo maarufu vya
habari hapa nchini.
Jembe hilo limeacha kazi rasmi Ijumaa ya tarehe 09-05-2014 kwa madai kwamba anakwenda kujiendeleza na masomo.
Jitihada
za kumpata Reuben Mchome mwenyewe ili kuthibitisha hili zilizaa matunda
Japo hakuwa tayari sana kulizungumzia suala hilo,ila baada ya kubanwa
na maswali alifunguka na kuzungumza.
Yafutayo ni mazungumzo yetu na mtangazaji huyo kijana ila mwenye kipaji cha hali ya juu,Reuben Mchome.
Eddy Blog-Mambo vipi Mchome.
Mchome-poa mambo vipi?
Eddy Blog-poa asee!! Nasikia umeacha kazi ITV,Ni kweli?
Mchome- Wee nani?
Eddy Blog-mwandishi wa habari wa Eddy blog!!
Mchome- wee nani kakwambia kama mimi nimeacha kazi?
Eddy Blog-Nimesikia watu wakiongea,Si uanajua nyie ni watu maarufu lazima mambo yenu yasambae kwa haraka!!
Mchome-sasa kama umesikia kwa watu unachotaka kwangu ni nini?
Eddy Blog-tunaomba ututhibitishie kama ni kweli au la!!?
Mchome- ni kweli nimeacha kazi
Eddy Blog-umefukuzwa au umeamua mwenyewe?
Mchome-(anaanza kwa kicheko) hapana sijafukuzwa nimeamua mwenyewe kuacha!!
Eddy Blog-umepata dili wapi?
Mchome-sijapata popote nimeamua kuacha ili nimalizie shule yangu.
Eddy Blog- ooooh!! Kumbe unasoma,unasoma wapi?
Mchome-Nipo chuo kikuu Tumaini
Eddy Blog-mwaka wa ngapi?
Mchome-wa tatu!!
Eddy Blog-kwahiyo ukimaliza utarudi kazini au ndio umetoka moja kwa moja?
Mchome-(anaanza kwa kicheko tena) hapana kaka siwezi kurudi tena!!
Eddy Blog-lakini inasemekana ulitofautiana kauli na "boss" wako ndio maana ukaamua kucha kazi ndani ya saa ishurini na nne!!
Mchome-(anastuka) Eh!! Wewe nani kakuambia hayo?
Eddy Blog-aaa kaka si unajua mwenyewe dunia siku hizi imekuwa kama kijiji!?
Mchome-
katika hilo kaka nakuomba sana usije ukanipandikizia maneno!! Mimi
sijatofautia na boss wangu yoyote pale, mimi nimeondoka kwa amani na
maboss wangu wote nimeagana nao kwa amani na upendo nakuomba sana kaka
unielewe hivyo!
Eddy
Blog- sawa kaka, ila kuna taarifa kwamba mkurugenzi wako Deogratius
Rweyunga alikukatalia likizo yako ya kwenda kufanya mitihani yako ndiyo
maana ukaamua kuacha kazi!!
Mchome-hayo
ni majungu kaka,wewe umesema umesikia kwamba nimeacha kazi ndio maana
ukaamua kunipigia kuthibitisha hilo,naomba uandike ninachokuambia mimi!! Sijanyimwa likizo wala sijatofautiana na aliyekua boss
wangu,huyo aliyekuambia ni mzushi na muongo!
Eddy Blog-lakini kaka inasemekana umepata dili kwenye kituo kimoja cha TV na Radio hapa nchini,ni kweli?
Mchome-sio kweli,sijapata dili na kwa sasa sitaki dili lolote hadi nitakapo maliza degree yangu mwezi wa saba.
Eddy Blog-lakini ukimaliza shule unatarajia kuendelea na kazi hii ya habari au ndio umeitema kabisa?
Mchome-dah sujajua kaka,unajua maisha ni hatua,ngoja nimalize shule kaka kitaeleweka tu.
Eddy Blog-basi naomba nikupe dili ukimaliza shule uje nikupatie ajira hapa Eddy Blog
Mchome-(anacheka kicheko kirefu) Poa poa kaka kama utakua na mkwanja wa kunilipa nitakuja usijali.
Eddy
Blog-poa kaka nashukuru kwa kuzungumza na Eddy Blog na tunakutakia kila
la kheri katika masomo yako na maisha mapya nje ya Radio one na ITV
Mchome-poa poa kaka tupo pamoja.
Hayo
yalikuwa mazungumzo kati yetu na Reuben Mchome,katika vituo hivyo
maarufu vya habari vya ITV na Radio One
Reuben Mchome kwa upande wa
Radio alikua anasoma taarifa za habari, kipindi cha Nipashe, Midundo
motomoto, Afrika Panorama, Breaking News na Uchunguzi kamili, kwa upande wa TV alikuwa
anasoma habari za michezo.
Eddy
Blog inamtakia Reuben Mchome kila la kheri katika masomo yake na
inawapa pole mashabiki na wapenzi wake ama kweli wataikosa sauti
iliyozoeleka masikioni mwao!!

