MFUKO WA PSPF WATOA TAHADHARI KWA WANACHAMA WAKE, KISA UTAPELI

TAARIFA KWA UMMA

Mfuko wa Pensheni wa PSPF unapenda kuwataarifu  wananchi wote kuwa, hivi karibuni kumekuwa na watu au kikundi cha watu wanaosambaza taarifa potofu kwa wanachama wa PSPF kwa njia ya ujumbe mfupi wa simu ya mkononi kwa nia ya kuwatapeli.


Taarifa hizo zinazotolewa siyo sahihi na PSPF inawaomba wanachama wake kuchukua tahadhari dhidi ya ujumbe huo wa kupotosha unaosambazwa kwa njia ya simu na watu au kikundi cha watu wakidai kuwa ujumbe huo unatoka PSPF.

PSPF inatoa huduma mbalimbali kwa wanachama wake bila sharti lolote wala malipo ya namna yoyote. Ujumbe wowote unaomtaka mwanachama kutuma fedha kwa ajili ya kulipia huduma yoyote inayotolewa na Mfuko siyo sahihi na ujumbe wa namna hiyo hautolewi na PSPF. Hivyo, ninawaomba wanachama wa PSPF kuwa makini na ujumbe huo unaosambazwa na watu wachache ambao wanataka kuuchafua Mfuko na kujinufaisha kwa njia zisizo halali.

Iwapo itatokea mwanachama amepata ujumbe wenye utata, tafadhali piga simu katika Kituo cha Huduma kwa Wateja wa PSPF kwa kutumia namba 022 5510400 au fika katika ofisi ya PSPF iliyopo karibu nawe au toa taarifa kituo chochote cha polisi kilicho karibu nawe kwa hatua stahiki.

Taarifa hii imetolewa na:
Mkurugenzi Mkuu
Mfuko wa Pensheni wa PSPF,
Makao Makuu, Golden Jubilee Towers, S. L. P. 4843, Dar-es-Salaam.
Simu: +255222120912/52 au +255222127375 /6
Nukushi: +255222120930
Barua pepe: pspf@pspf-tz.org
Tovuti: www.pspf-tz.org
 www.facebook.com/PSPFTanzania
  @Pspf_Tanzania


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo