Meneja
wa Bia ya Kilimanjaro George Kavishe akiongea na waandishi wa Habari
muda mfupi juu ya mchakato mzima wa tuzo za Kili Music Awards 2013-
2014, ndani ya Jengo la kampuni hiyo lililopo Masaki jijini Dar es
Salaam.
KAMPUNI Bia ya TBL inayozalisha kinywaji cha Kilimanjaro, leo imeweka
wazi juu ya mwenendo wa shindano lake la Kili Music Awards ambalo
linaendelea kwa sasa nchini kwa kuwapa fursa watanzania kuwapigia kura
wasanii wa Muziki nchini katika vipengele vya tuzo hizo.
Meneja wa Kinywaji hicho, George Kavishe amesema kwamba baada ya
Watanzania kupendekeza wasanii kwa mujibu wa vigezo vya BASATA na
Academy,kupigia kura wateule kwenye vipengele hivyo sasa watanzania
wanatakiwa kupiga kura za mwisho ili kukamilisha asilimia 70
zinazotarajiwa kupatika kutoka kwa wapenzi wa muziki huo.
Aidha Kavishe aliweka wazi kwamba mchakato wa upigaji kura
unatarajiwa kufungwa itakapofikia tarehe 30 mwezi huu na baada ya hapo
wasanii na mashabiki wao watakutana kwa pamoja tena tarehe 3 mwezi wa
tano mwaka huu, ambapo itakuwa ndiyo siku rasmi ya washindi kukabidhiwa
tuzo zao.
“Naomba watazania wapige kura kwa wingi maana hii ndiyo wiki ya mwisho ya kumpatia kura msanii uanayempenda, maana ukishindwa kufanya hivyo ndani ya wiki hii utakuwa umepoteza haki yako ya msingi kwani zoezi hili linatarajiwa kufungwa mara moja itakapofika tarehe 30 mwezi huu,” alisema Kavishe.
(Habari/Picha: Musa Mateja/GPL.)