HALMASHAURI YA WILAYA YA IRINGA YAWAFUKUZA KAZI WATUMISHI WALIOTOROKA KAZINI

 
Na Bongo leaks
HALMASHAURI ya wilaya ya Iringa imewafukuza kazi watumishi wake sita, kutokana na makosa mbali mbali ikiwemo utovu wa nidhamu na utoro kazini.

Maamuzi hayo yamefikiwa katika kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo, baada ya watumishi hao kwa nyakati tofauti kupewa onyo na kalipio kali.

Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Steven Mhapa alisema katika kipindi chote cha utovu wa nidhamu watumishi hao waliendelea kupokea mishahara yao kama kawaida.

“Ofisi ya Mkurugenzi ilileta rasmi ombi la kuwafukuza kazi watumishi hawa, hivyo baraza la madiwani limebariki kwani, hata sisi hatupo tayari kuona kazi zinalala kwa sababu za uvivu,” alisema
 
Aliwataja watumishi hao kuwa ni Andrew Mtavangu na Uswege Mwakosya waliokuwa Maafisa Elimu Wasaidizi Daraja la Tatu na Prosper Mzena aliyekuwa Mwalimu.
 
Wengine ni Sabath Masembo aliyekuwa Afisa Mtendaji wa Kata Daraja la Pili, Abdukadh Mnyavanu aliyekuwa Mtendaji wa Kijiji na Godfrey Msuya aliyekuwa Tabibu Msaidizi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo