NDEGE YA MALAYSIA ILIANGUKA BAHARI YA HINDI NA KUSABABISHA VIFO VYA ABIRIA WOTE WALIOKUWEMO KATIKA NDEGE HIYO

http://i2.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2014/03/Screen-Shot-2014-03-17-at-11.49.52-PM.png
 
Waziri mkuu wa Malaysia Najib Razak.

 
Waziri Mkuu wa Malaysia, Najib Razak, amesema data mpya zinaonyesha kuwa ndege ya nchi hiyo iliyopotea  imeangukia kusini mwa Bahari ya Hindi. 

Razak amesema taarifa hizo zimeonyesha kuwa eneo la mwisho la ndege hiyo ilikuwa katikati mwa Bahari ya Hindi, magharibi mwa mji wa Perth, Australia. 

Amesema eneo hilo liko ndani ndani na liko mbali na uwanja wowote ule wa ndege.

Amesema kulingana na data hizo mpya, ndege nambari MH 370 iliangukia kusini mwa Bahari ya Hindi. Razak amesema taarifa zaidi kuhusu data hizo mpya, zitatolewa kesho Jumanne.
via>>dw swahili


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo