PINDA: VIONGOZI WA DINI WANA NAFASI KUBWA YA KUTATUA MIGOGORO YA ARDHI

Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema viongozi wa dini wana nafasi kubwa ya kumaliza changamoto ya migogoro ya ardhi nchini kutokana na wananchi kuwa na imani nao zaidi kuliko viongozi wa serikali na wanasiasa.

Amesema umefika wakati kwa viongozi hao kutumia imani hiyo ya kusikilizwa na wananchi kupata suluhu la migogoro ya ardhi pamoja na kuondoa matabaka baina ya wafugaji na wakulima yaliyosababishwa na mi
gogoro hiyo.

Ni katika Uzinduzi wa Jukwaa la Ardhi Tanzania ndipo Waziri Pinda anasema jitihada za ziada zinahitajika kutoka kwa viongozi hao kutatua migogoro hiyo ya ardhi.

Ameongeza kuwa kuna umuhimu wa kushirikiana zaidi kulinda amani kwa mustakabali wa maendeleo ya nchi.

Kwa Upande wake Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kirutheri Tanzania KKKT Dk. Alex Malasusa anasema kuna haja ya kuweka mipango mizuri ya usimamizi wa ardhi kutokana na idadi ya watu wenye mahitaji ya ardhi kuongezeka kila siku.

Jukwaa la Ardhi Tanzania limeshirikisha viongozi wa dini ya Kiislamu na kikristo, serikali, asasi za kiraia na wadau mbalimbali ambapo miongoni mwa majukumu yake ni kutafuta suluhu la migogoro ya ardhi nchini kupitia ushirikishwaji wa jamii husika kufanya maamuzi yenye lengo la kudumisha amani ya nchi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo