MKUU WA MKOA IRINGA AZUNGUMZA NA WAFANYABIASHARA BAADA YA KUGOMEA MASHINE ZA TRA JANA MKOANI HUMO



duka_1_63817.jpg
Mkuu wa mkoa wa Iringa, Dr. Christina Ishengoma leo amezungumza na wafanya biashara wa manispaa ya Iringa katika ukumbi wa community centre uliopo eneo la Kitanzini katika manispaa ya Iringa, mada kuu ilikuwa inahusu mgomo wa wafanya biashara kupinga mashine mpya za kutoa risiti zilizotolewa na TRA ili zitumike katika biashara zao.
duka_2_19543.jpg
baadhi ya wafanya biashara walio hudhuria katika mkutano huo uliofanyika leo.
duka_9_e1545.jpg
Mwenyekiti wa TCCIA mkoa wa Iringa,Bw. Lucas Mwakabunge, akizungumza na wafanya biashara katika mkutano huo.
duka_5_a19b2.jpg
duka_3_dc400.jpg
Pichani ni baadhi ya Wafanyabiashara wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa katika mkutano huo.

Mkuu wa mkoa huyo alisisitiza kuwa elimu inatakiwa kutolewa kwa wafanya biashara hao kuhusu umuhimu wa mashine hizo kwa kuwa wafanya biashara wengi wameonesha hali ya kutoridhishwa nazo na hata kufanya maandamano ya nchi nzima wakipinga matumizi ya mashine hizo na kutaka kendelea kutumia mfumo wao wa zamani wa kutumia vitabu.

Mkuu wa mkoa huyo alidai kuwa yeye sio muhusika mkuu wa suala hilo lakini kama ilivyo, ni wajibu wake kuzungumza na hata kuwasaidia watu wake hivyo aliwataka wafanya biashara hao fungua maduka kwani kilio chao kimesikika na serikali inalifanyia kazi suala hilo.
PICHA ZAIDI INGIA MJENGWA BLOG.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo