MAMA ASHAURIWA AMNYWESHE MWANAYE SUMU AFE HUKO TABORA, KISA KAUGUA MUDA MREFU



Mtoto Tatu Hassan akiwa mwenye furaha na mama yake mzazi Bi. Halima Mgelwa, mtoto huyu amekuwa kitandani kwa zaidi ya miaka kumi na moja kutokana na maradhi ya kichwa kujaa maji huko katika kijiji cha Magiri wilayani Uyui mkoani Tabora.


Mama wa mtoto huyu anaomba msaada wa matibabu kwa wasamalia wema,tatizo kubwa kichwa cha mtoto huyu kimejaa maji na hivyo anahitajika kupelekwa hospitali ya Bungando jijini Mwanza.


Mama huyu kwa mujibu wa maelezo yake amekuwa akilazimika kumfungia ndani ya nyumba kila siku na kwenda kutafuta riziki kwa muda wote huo wa miaka kumi na moja na hivyo hata baadhi ya majirani zake wa karibu hawatambui kama kuna mtoto huyu hapo kijijini.

Jambo baya zaidi baadhi ya watu wenye imani potofu walithubutu kumshawishi mama huyu aweze kumpa SUMU mtoto wake eti kwa madai kwamba amekuwa akihangaika sana kumuhudumia


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo